Kundvagn 0
Kundvagn 0
 

Karatasi ya maelezo - Ualbino Tanzania

Ualbino ni hali ya kijenetiki inayosababisha ukosefu wa rangi ya asili katika ngozi na nywele, pamoja na uoni hafifu. Ualbino sio ugonjwa na wala hauambukizwi. Mtu mwenye ualbino sio kwamba amelaaniwa na wala sio zimwi, bali ni binadamu. Bila kujali kabila la mtu, mama na baba wasio na ualbino wanaweza kupata mtoto mwenye ualbino.

Watu wengi wenye ualbino Tanzania wanakabiliwa na madhara ya fedheha pamoja na ukandamizwaji kutokana na muonekano wao. Baadhi ya watoto wenye ualbino wanaonewa shuleni, wengine wanatelekezwa na familia zao. Watu wazima wenye ualbino wanaweza kuhangaika kukidhi mahitaji yao kwa sababu hawatakiwi kukaa kwenye jua kutokana na hatari ya kupata kansa ya ngozi. Katika baadhi ya maeneo, watu wenye ualbino wamekuwa wakishambuliwa kikatili, na wengine hata kuuawa.

 
 

Ukiwa kama binadamu mwenzao, unao wajibu mkubwa wa kufanya maisha ya watu wenye ualbino kuwa salama na ya haki. Unaweza kusaidia kwa namna zifuatazo:

 
 

Kama ni mwalimu:

Mruhusu mtoto mwenye ualbino kukaa mbele ya darasa kutokana na uoni hafifu.

  • Msaidie na umkumbushe mtoto mwenye ualbino kuepuka jua kwa sababu linaweza kupelekea kubabuka kwa ngozi, kitu kinachoweza kusababisha kansa ya ngozi.

  • Mruhusu mtoto mwenye ualbino kuvaa sare za shule zilizoboreshwa kama vile nguo za mikono mirefu, suruali, sketi ndefu na kofia kwa ajili ya kukinga ngozi yake isibabuke na jua.

  • Chochea umoja na muunganiko miongoni mwa wanafunzi, kwa wanafunzi wote.

Kama ni shirika lisilo la kiserikali au mtu anayefanya kazi na jamii:

  • Saidia miradi midogo au mikubwa inayohusisha watu wenye ualbino na kuwajengea uwezo.


Kama ni mwajiri:

  • Tengeneza mazingira ya kazi yawe rafiki kwa kila mtu, na pia toa fursa za ajira kwa watu wote ikiwa ni pamoja na watu wenye ualbino.

Kama ni kiongozi:

  • Wasemee watu wote – wewe ni kioo chao.

  • Zuia uenezwaji wa taarifa za uongo au uvumi hatarishi kuhusu watu wenye ualbino.

  • Zingatia haki za binadamu kwa watu wote.

 

Kwa pamoja tunaweza kuonyesha kuguswa, kisha kuongeza uelewa miongoni mwa jamii na kuhakikisha sauti za watu wenye ualbino zinasikika na kuheshimiwa. Kila mtu ana haki ya kuishi katika hali ya usalama na utu.

 
 

Unataka kujua zaidi au kushirikiana nasi?

Wasiliana nasi kupitia fomu iliyo hapa chini au piga simu kwa Sr. Martha Martha Mganga - mwanzilishi wa NGO ya Tanzania ya Peacemakers for Albinism and Community +255 754 511 828